-
Hadiyth
عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو بْن الْعاص (رضي الله عنهما) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ َقَالَ: ((الْكَبَائِرُ الإِشْرَاكُ بِاللَّهِ, وَعُقُوقُ الْوَالِدَيْنِ, وَقَتْلُ النَّفْسِ وَالْيَمِينُ الْغَمُوسُ)) البخاري وفي رواية لَهُ: أنَّ أَعْرَابِياً جَاءَ إِلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّه,ِ مَا الْكَبَائِر؟ ُ قَالَ: ((الإشْرَاكُ بِاللَّهِ)) قَالَ: ثُمَّ مَاذَا؟ قَالَ: ((الْيَمِينُ الْغَمُوسُ)) قُلْتُ: وَمَا الْيَمِينُ الْغَمُوسُ؟ قَالَ: ((الَّذِي يَقْتَطِعُ مَالَ امْرِئٍ مُسْلِمٍ!)) يَعْنِ: بِيَمِينٍ هُوَ فِيهَا كَاذِبٌ
Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amri bin Al-‘Aasw (رضي الله عنهما) amesema kuwa Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم ) amesema: (Madhambi makubwa ni kumshirikisha Allaah, Kuwaasi wazazi wawili, Kuua nafsi na yamini [kiapo] ya uongo)).
Na katika riwaaya nyingine: “Alikuja Mbedui mmoja kwa Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) akamuuliza: Ee Mjumbe wa Allaah? Ni yepi madhambi makubwa? Akasema: ((Kumshirikisha Allaah)) Akasema: Kisha yepi? Akasema: ((Yamini ya uongo)). Nikauliza: Ni ipi yamini ya uongo? Akasema: ((Ni ambayo mtu hujichukulia mali ya Muislamu!)) yaani akaapa kwa uongo.
Blogger Comment